TANGAZO

TANGAZO
WEKA TANGAZO LAKO HAPA

Jumamosi, 28 Septemba 2013

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda anatarajiwa kufungua Kongamano la siku mbili la Uwekezaji kanda ya Kaskazini kesho



wwwbinhafidhi.blogspot.com

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda anatarajiwa kufungua Kongamano la siku mbili la   Uwekezaji kanda ya Kaskazini kesho pamoja na maonyesho ya kibiashara na Utalii ambapo wageni wa ndani na nje ya nchi wanatarajiwa kuhudhuria.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa alisema Pinda anatarajiwa kuwasili kesho (leo) ambapo jumla ya wageni 450 wanatarajiwa kuhudhuria.

Alisema Kongamano hilo la siku mbili litashirikisha halmashauri 33 za kanda ya Kaskazini ambapo kila moja itajifunza na kueleza namna ambavyo halmashauri yake inavyoendeshwa.

“Waziri Mkuu Mizengo Pinda ndie atakaeongoza kongamano letu la siku mbili pamoja na kufungua maonyesho ya kibiashara—hii  ni fursa nzuri ya  wenye viwanda na biashara kujitangaza” alisema na kuongeza

“Kongamano hili litakuwa na mapinduzi kwa halmashauri zetu hasa kwa hii kanda ya kaskazini kwani baada ya hapo tunataka kufanya kazi kwa vitendo na sio kwa nadharia” alisema Gallawa

Gallawa alisema kongamano hilo ambalo lengo lake ni kuwashawishi wawekezaji kujionea fursa zilizopo za uwekezaji kanda ya kaskazini  pamoja na miundombinu mizuri ya kusafirisha bidhaa kwa kutumia barabara, reli na bandari zikiwa zinapatikana.

Alisema Mikoa ya kanda ya Kaskazini iko na fursa nyingi za uwekezaji lakini inashindwa kujitangaza na hivyo kuonelea kuitisha kongamano hilo pamoja na wawekezaji kujionea wao wenyewe.

“Mimi nadhani baada ya kongamano hili wawekezaji watajua kuwa kweli eneo letu linafaa kwa uwekezaji na ninaamini maisha ya wananchi yatabadilika na umasikini utapungua” alisema Gallawa

Alisema kongamano hilo ambalo litaenda sambamba na maonyesho ya biashara na kazi za asili zinazotengenezwa  ndani na kuwataka wananchi kujifunza kupitia kongamano hilo ambalo ni nafasi adhimu kwao na kwa Mk

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni