TANGAZO

TANGAZO
WEKA TANGAZO LAKO HAPA

Jumapili, 29 Septemba 2013

‘Hatari ya silaha za nyuklia za Israel izingatiwe’


‘Hatari ya silaha za nyuklia za Israel izingatiwe’


Msemaji wa Jumuiya ya Kiislamu ya Colombia amesema kuwa, walimwengu wanapaswa kuzingatia hatari ya silaha za atomiki za utawala wa Kizayuni wa Israel. Rashid Caravali amesisitiza kwamba, umewadia wakati sasa kwa nchi za Mashariki ya Kati na nchi nyingine ulimwenguni kuipa uzito hatari ya silaha za nyuklia za utawala haramu wa Israel hasa kwa kuzingatia kwamba, utawala huo mara kadhaa wa kadhaa umeonesha wazi na bila kificho uadui wake kwa nchi za eneo. Msemaji wa Jumuiya ya Kiislamu ya Colombia ameongeza kuwa, Israel sio tu kwamba, inamiliki silaha za kemikali bali inazo pia silaha za nyuklia ambazo ni tishio kubwa kwa usalama wa dunia hususan eneo la Mashariki ya Kati. Rashid Caravali amesema, jamii ya kimataifa inapaswa kuushinikiza utawala huo ghasibu ili uangamize silaha zake zote za atomiki na kwa muktadha huo eneo la Mashariki ya Kati litashuhudia amani na utulivu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni