TANGAZO

TANGAZO
WEKA TANGAZO LAKO HAPA

Jumapili, 29 Septemba 2013

Al-Mualim: Mpango amani umshirikishe Assad

Al-Mualim: Mpango amani umshirikishe Assad



Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria amesema kuwa, serikali ya Damascus haitokubali mpango wowote wa amani wa kukabidhi madaraka kwa ajili ya nchi hiyo ambao hautomshirikisha Rais Bashar al Assad.
Akizungumza pambizoni mwa mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Walid al Muallim ameongeza kuwa, kwa wananchi wa Syria Bashar ni Rais aliyechaguliwa kuongoza nchi hadi katikati ya mwaka ujao wa 2014, ambapo uchaguzi mwingine wa rais utafanyika. Ameongeza kuwa, serikali ya Damascus itawakaribisha wagombea wengine kushiriki uchaguzi huo kwa mujibu wa katiba na kwamba taifa la Syria ndilo lililo na haki ya kuchagua kiongozi wake.
Aidha Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria amesema, magaidi wanaopigana nchini humo wanaungwa mkono na nchi jirani kama Uturuki na Jordan pamoja na baadhi ya nchi za Kiarabu kama vile Saudi Arabia na Qatar.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni