TANGAZO

TANGAZO
WEKA TANGAZO LAKO HAPA

Jumamosi, 12 Oktoba 2013

Wakimbizi wengine wazama baharini


Wakimbizi kadhaa wanahofiwa kuwa wamekufa baada ya  mashua yao kuzama karibu na kisiwa cha Sicily, katika bahari ya Mediterenia nchini Italia.

 Watu 250 wanasemekana kuwa walikuwamo katika mashua  hiyo iliyozama umbali wa maili 70, kutoka pwani ya kisiwa cha Italia cha Lampedusa.

 Shirika la Habari nchini Italia Ansa limesema takribani miili 50, ikiwa ni pamoja na wanawake na karibu watoto 10, imeondolewa baharini. 

Waziri Mkuu wa Italia Enrico Letta amesema kiasi ya manusura 150 wameokolewa na meli nyingine ya Malta. 

Wiki iliyopita wakimbizi zaidi ya mia  tatu  walikufa maji karibu na  kisiwa hicho cha Lampedusa. 

Mashua  hiyo  iliyokuwa inawasafirisha wakimbizi mita tano ilizama baada ya kuwaka  moto.

Idadi kubwa ya  wakimbizi   walikuwa wanatoka  Eritrea na  Somalia.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni