TANGAZO

TANGAZO
WEKA TANGAZO LAKO HAPA

Jumamosi, 5 Oktoba 2013

Shughuli za uokoaji zasimamishwa Lampedusa


Zaidi ya watu miamoja kumi na watu wamepatikana wakiwa wamekufa maji na wengine miambili bado hawajulikani waliko

Hali mbaya ya hewa imewasababisha waokoaji kuahirisha juhudi za kutafuta miili ya wahamiaji zaidi ya 200 ambao hawajulikani waliko, baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kushika moto na kuzama karibu na kisiwa cha Lampedusa, kusini mwa Italia. Wapiga mbizi walifanikiwa kuipata miili zaidi ya 100 ya wahamiaji huku watu zaidi ya 150 wameokolewa. Inaaminika boti hiyo iliopinduka ilikuwa na wahamiaji takriban 500 waliokuwa wanatokea nchini Somalia na Eritrea. Kamishna wa Umoja wa Ulaya  anayeshughulika na maswala ya  ndani  Cecilia Malmstroem, ameapa kuwa atapambana na watu wanaosafirisha  watu kwa  njia  haramu  kwa kutumia hali  yao  mbali  ya maisha. Italia  ilitangaza  siku  moja  ya  maombolezo  jana  Ijumaa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni