TANGAZO

TANGAZO
WEKA TANGAZO LAKO HAPA

Jumatatu, 21 Oktoba 2013

Watu watatu akiwemo msichana mdogo mwenye umri wa miaka 8 wauawa

Waumini walishambuliwa wakiwa wanatoka kanisan
Watu watatu akiwemo msichana mdogo mwenye umri wa miaka 8 aliuawa wakati watu waliokuwa wamejihami wakiwa kwenye pikipiki kushambulia sherehe za ndoa nje ya kanisa la Kikopti mjini Cairo.

Boko Haram waua madereva 19 Nigeria

Mabaki ya magari ya madereva waliouawa na Boko Haram
Wanamgambo waliokuwa wamevaa nguo za kijeshi, wamewaua watu 19 katika kuzuizi cha barabarani walichokuwa wameweka kukagua magari katika jimbo la Borno.

Jumapili, 13 Oktoba 2013

Utaliana itazidisha doria Mediterranean

Wanajeshi wakisaidia katika uokozi, Lampedusa
Utaliana itazidisha doria za wanajeshi kusini mwa bahari ya Mediterranean, baada ya mamia ya wakimbizi kuzama

Upinzani wa Syria hautaki kuzungumza

George Sabra
kongozi wa kundi kubwa katika ushirikiano wa upinzani nchini Syria amesema ana hakika hatohudhuria

Hijja yaanza Makka


Malaki  ya waumini wamekusanyika Mina karibu na mji wa Saud Arabia wa Makka kuanza kutekeleza nguzo ya tano ya dini ya kiislam-Hajji.

HIVI HAWA BAKWATA WANA AKILI AU MATOPE AU NI MAKAFIRI????

Jamani waislamu tusipelekwe tu kama magari mabovu na hawa bakwata kwasababu sijui niwaweke katika kundi gani yaani hawana hata aibu wanatangaza edd jumatano haliya kua watu wana simama arafa kesho waislamu tuamke tuacheni kulala jamani.



hii ndo taarifa yao hebu isome. chanzo bakwata.

Jumamosi, 12 Oktoba 2013

Wakimbizi wengine wazama baharini


Wakimbizi kadhaa wanahofiwa kuwa wamekufa baada ya  mashua yao kuzama karibu na kisiwa cha Sicily, katika bahari ya Mediterenia nchini Italia.

Ijumaa, 11 Oktoba 2013

Pinda ampiga stop Magufuli ni mara baada ya meli, mizigo kukwama bandarini

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ametengua maamuzi yaliyofanywa na Waziri wa Ujenzi Dk. John Magufuli ya kuongeza tozo ya asilimia tano kwa wasafirishaji wa malori na mabasi kwa uzito unaozidi.

Ajali ya moto ya ua watu kumi nchini japani

10 wafariki katika ajali ya moto ndani ya hospitali Japan

hebu skia hjii heti wabakaji nchini kenya adhabu yaokukata nyasi

Mwathiriwa alisema kuwa anawajua wabakaji
Wakenya wameghadhabishwa sana na hatua ya wanaume watatu waliombaka msichana mmoja na kutupa mwili wake kwenye choo kuamrishwa na polisi kukata nyasi kama adhabu kwao.

JK: Tunataka malaria ikome mwaka 2016


Rais Jakaya Kikwete, amesema ni dhamira ya Tanzania kuhakikisha kwamba malaria inatokomezwa kabisa hapa nchini ifikapo mwaka 2016.

AU kujadili uhusiano wake na ICC

AU inajadili swala hili baada ya ICC kupuuza ombi la kutaka kuhamisha kesi za Kenyatta na Ruto
Marais wa Afrika wanakutana wikendi hii mjini Addis Ababa nchini Ethiopia kujadili uhusiano wa bara la Afrika na mahakama ya kimataifa ya jinai ICC.

Rais Banda awafuta kazi mawaziri kwa ufisadi

Rais Banda amewafuta kazi mawaziri wake wote kutokana na ufisadi
Rais wa Malawi, Joyce Banda amelifuta kazi baraza lake la mawaziri kutokana na kuongezeka kwa visa vya ufisadi serikalini.
Maafisa wa serikali wamekuwa wakipatikana na pesa zikiwa zimefichwa chini ya vitanda vyao na kwenye magari yao, kwa mujibu wa mwandishi wa BBC Raphael Tenthani.

Alhamisi, 10 Oktoba 2013

Taliban tayari kwa mazungumzo Pakistan

Taliban wako tayari kwa mazungumzo ila wataendelea kushambulia maslahi ya Marekani

Kiongozi wa Taliban nchini Pakistan Hakimullah Mehsud ameambia BBC kuwa yuko tayari kwa mazungumzo na serikali ingawa amesisitiza kuwa bado serikali haijamshauri.

Marekani kubana msaada wa kijeshi Misri

Marekani intaka Misri kuhakikisha uchaguzi huru na haki unafanyika kabla ya kuipa msaada tena
Marekani inabana sehemu kubwa ya dola bilioni 1.3 ambazo hutolewa kwa Misri kama msaada wa kijeshi.

Jumanne, 8 Oktoba 2013

peruuuuzi na kdadisi magazeti ya bongo ya leo j,4 octoba 13

 
 

Wanajeshi watano wauawa Misri

Kuna wasiwasi kuwa wanajeshi na vikosi vya usalama vinalengwa kwa mashambulizi la Misri
Watu waliojihami nchini Misri wamewaua wanajeshi watano katika eneo la Mkondo wa Suez mjini Ismailiya.

Lampedusa: Miili 232 imepatikana

Wanajeshi wakisaidia na juhudi za kuokoa maiti
Wapiga mbizi nchini Utaliana wamapeta idadi kubwa ya maiti katika boti iliyozama na ambayo ilikua imewabeba wahamiaji wa kiafrika kwenda Ulaya siku ya Alhamisi.

Jumapili, 6 Oktoba 2013

Maiti zaidi zapatikana Lampedusa

Kazi za uokozi zaanza tena Lampedusa

Wakuu wa Utaliana katika kisiwa cha Lampedusa wanasema wameopoa miili zaidi kutoka meli iliyozama Alkhamisi.

Maadhimisho ya vita yauwa zaidi Misri


Mtu aliyejeruhiwa katika maandamano ya Misri
Watu kama 15 wameuwawa kwenye mapambano nchini Misri wakati wafuasi wa rais wa Kiislamu,

CUF,NCCR Mageuzi,Chadema, wakubaliana na JK

Rais Jakaya Kikwete
Vyama vya Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi , vimekubali ushauri wa Rais Jakaya Kikwete wa kutaka hoja ya

hebu cheki hii ajali hapa katika video wanafunzi wa nusurika kufa jijini dar

tazama hapa sasa tukio lenyewe la ajali jinsi ilivyo kua


Kenya yatangaza majina ya magaidi


Serikali ya Kenya imetaja majina ya watu 4 waliofanya shambulizi la kigaidi kwenye jengo la kibiashara la Westgate mjini Nairobi, na kutoa picha za video zinazowaonyesha magaidi hao ndani ya jengo walilolishambulia.
Mtafaruku ndani ya jengo la Westgate siku ya mashambulizi
Mtafaruku ndani ya jengo la Westgate siku ya mashambulizi

arekani yaingia Barawe na Tripoli

Anas al Libi

Waziri wa Mashauri ya nchi za Nje wa Marekani, John Kerry, amesema kuwa mashambulio yaliyofanywa na

MTOTO WA AJABU AZALIWA ZANZIBAR!


MTOTO WA AJABU AZALIWA ZANZIBAR, AANZA KUONGEA AKIWA NA MIEZI MIWILI TU. MAMA AMFIKISHA KWA VIONGOZI NA KUFUNGUKA MAKUBWA. SOMA HAPA


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgTTgDBnGW9SX4geMuOwRYLxCUpy7IGbfKvfPNZwBlssTDU_DSmKwscR5p5vYUJy1IEAKntyf5XomegC6f-YPLW8qlodzLJ_4xokTf0xaxv47eLQQF3QS7DytRpD1DycGSp-719IwacmA/s640/Capture.JPG



MTOTO wa miezi 10, aliyetambuliwa kwa jina la Fahazal mkazi wa Kivunge amefikishwa mbele ya serikali ya mkoa wa kaskazini Unguja, baada ya mama yake mzazi kusema amekuwa akitokewa na maajabu na kwamba jamii iombe dua ili kunusuru kutokea vifo.

Ungereza na Uturuki zakana kua hazikuvamia Barawe

Wapiganaji wa al-Shabaab nchini Somalia
Wanachama wa kundi la al-Shabaab nchini Somalia wanasema kuwa mji wao kusini mwa Somalia umeshambuliwa na wanajeshi wa mataifa ya Magharibi.

Jumamosi, 5 Oktoba 2013

Serikali yatangaza nafasi za kazi 1,100


Serikali kupitia Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma imetangaza nafasi za kazi 1,134 katika sekta mbalimbali za ofisi za umma.

yombo vya habari sasa kuminywa zaidi


Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika akizungumza na waandishi wa habari makao makuu ya chama hicho, jijini Dar es Salaam, jana. PICHA | FIDELIS FELIX 
Dar es Salaam.  
Siku sita baada ya Serikali kuyafungia magazeti ya Mwananchi na Mtanzania kwa madai ya

Rais jakaya agongelea msumari wa mwisho kwa vya vyasiasa kuhusina na mchakato wa katiba mpya

Rais Jakaya Kikwete

*Apinga maandamano ya wapinzani
*Awakaribisha Ikulu kwa majadiliano
*Amshushua Tundu Lissu, asema mzushi
*Kuvunjwa Tume ya Warioba afafanua

Rais Jakaya Kikwete, amekata mzizi wa fitina katika suala la mchakato wa katiba kwa kushauri ile hoja ya Kamati ya Bunge ya Katiba

Obama afuta ziara yake barani Asia



Rais wa Marekani Barrack Obama amefuta ziara yake barani Asia na pia hatohudhuria mikutano miwili ya kimataifa kutokana na kufungwa kwa shughuli za serikali ya Marekani.

Watu wanne wauwawa Mombasa

Kenya

Watu wanne wamethibitishwa kuuwawa baada ya makabiliano makali kati ya polisi na waandamanaji mjini Mombasa kenya walioandamana hapo jana baada ya Sala ya Ijumaa kupinga kuuwawa kwa Sheikh Ibrahim Ismail

Shughuli za uokoaji zasimamishwa Lampedusa


Zaidi ya watu miamoja kumi na watu wamepatikana wakiwa wamekufa maji na wengine miambili bado hawajulikani waliko

Hali mbaya ya hewa imewasababisha waokoaji kuahirisha juhudi za kutafuta miili ya wahamiaji zaidi ya 200 ambao hawajulikani waliko, baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kushika moto na kuzama karibu na kisiwa cha Lampedusa, kusini mwa Italia. Wapiga mbizi walifanikiwa kuipata miili zaidi ya 100 ya wahamiaji huku watu zaidi ya 150 wameokolewa. Inaaminika boti hiyo iliopinduka ilikuwa na wahamiaji takriban 500 waliokuwa wanatokea nchini Somalia na Eritrea. Kamishna wa Umoja wa Ulaya  anayeshughulika na maswala ya  ndani  Cecilia Malmstroem, ameapa kuwa atapambana na watu wanaosafirisha  watu kwa  njia  haramu  kwa kutumia hali  yao  mbali  ya maisha. Italia  ilitangaza  siku  moja  ya  maombolezo  jana  Ijumaa.

Wafuasi wa Morsi wakabiliana na polisi Misri


Idadi kubwa ya wafuasi wa Morsi wamezuiliwa na wengine kuuawa
Vikosi vya usalama nchini Misri vimeimarisha ulinzi katika sehemu kadhaa mjini Cairo baada ya vurugu kuzuka kutokana na makabiliano kati ya wafuasi wa Mohammed Morsi na vikosi vya usalama katika mji huo na ule wa Alexandria.

Mambo Shuari Rwanda na TZ, asema Kikwete

Rais wa TZ , Jakaya Kikwete
Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete ametangaza kuwa mgogoro baina ya Tanzania na Rwanda umemalizika.
Katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi kwa raia wa nchi hiyo Rais Kikwete amesema hatua hiyo inafuatia mazunguzo baina ya viongozi hao wawili yaliyofanyika hivi karibuni nchini Uganda

Ijumaa, 4 Oktoba 2013

Rwanda yakosoa vikwazo vya Marekani dhidi yake


Jeshi la Rwanda limekosoa vikali vikwazo vilivyowekwa na Marekani dhidi ya nchi hiyo. Taarifa zinasema kuwa, Marekani imechukua uamuzi huo baada ya kulituhumu jeshi la Rwanda kuwa liliwasaidia waasi wa M23 wa Kongo katika kuwatumikisha watoto jeshini.

Juhudi za uokozo zaendelea Lampedusa

Baadhi ya waliopoteza maisha yao wakitafuta kuingia Ulaya
Juhudu za uokozi zimeanza tena Kusini mwa Utaliano baada ya boti iliyokuwa imewabeba wahamiaji wa kiafrika kwenda Italia, kuzama katika kisiwa cha Lampedusa.

Muhubiri wa kiisilamu auawa Mombasa

Marehemu Aboud Rogo alidaiwa kuwa na uhusiano na kundi la kigaidi la Al Shabaab
Kiongozi mmoja wa dini ya kiisilamu ameuawa kwa kupigwa risasi pamoja na watu wengine mjini Mombasa, Pwani ya Kenya.

Mazungumzo ya kitaifa Tunisia kuanza kesho

Tunisia

Duru ya kwanza ya mazungumzo ya moja kwa moja kati ya chama tawala cha an Nahdha nchini Tunisia na vile vya upinzani yenye lengo la kutatua mivutano ya kisiasa, itaanza hapo kesho nchini humo

jimbo jingine Ujerumani lautambua rasmi Uislamu

Ujerumani








Jimbo la Niedersachsen moja kati ya majimbo 16 nchini Ujerumani, limeitambua dini ya Kiislamu kuwa ni dini rasmi kwenye jimbo hilo lililoko kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.

13 wafariki katika ajali ya ndege Nigeria



Ndege
Ndege iliyokuwa imewabeba watu 27 imeanguka baada ya kukumbwa na hitilafu ya injini, muda mfupi baada ya kuruka kutoka uwanja wa ndege mjini Lagos

Alhamisi, 3 Oktoba 2013

Mkutano wa vijana kufanyika SA

Vijana nchini Afrika Kusini wakiadhimisha siku ya vijana duniani
Kile kinachosemekana kuwa mkutano mkubwa zaidi wa vijana unatarajiwa kuanza hivi punde mjini Johannesburg nchini Afrika Kusini.

Uchunguzi wa DNA kwa viungo vya miili Kenya

Chumba cha kuhifadhia maiti cha baraza la jiji la Nairobi
Jamaa ya baadhi ya wakenya waliopotea kufuatia shambulizi la kigaidi la Westgate wamejitokeza kufanyiwa uchunguzi wa chembechembe za DNA.
Polisi walitoa ombi hilo baada ya kupata viungo vya mwili katika jengo hilo

Kibali cha ICC kumkamata mwandishi Kenya


Walter Barasa

Mahakama ya kimataifa ya ICC, imetoa kibali cha kukamatwa kwa raia Mkenya ambaye anatuhumiwa kwa kujaribu kuwahonga mashahidi ili wajiondoe kwenye kesi dhidi ya Naibu Rais wa Kenya William Ruto.

Jumatano, 2 Oktoba 2013

Marekani - Funga afisi, hakuna pesa

Afisi zimefungwa. hakuna pesa
Serikali ya Marekani imeamkia Jumanne kwa pigo kubwa ya kufunga baadhi ya afisi za umma kutokana na ukosefu wa fedha za kuziendesha.

ICC yamsaka mshirika wa Gbagbo

Bwana Ble anashukiwa kufanya mauaji, ubakaji, mateso na vitendo vingine vya kinyama

Mahakama ya kimataifa ya ICC, imetangaza rasmi kutoa kibali cha kumkamata aliyekuwa waziri wa Ivory Coast,Charles Ble Goude kwa madai ya uhalifu wa kivita

Kenya - Bila usalama Somalia, hatutoki !


Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta atoa Onyo kali kwa magaidi

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ametangaza kuwa majeshi ya Kenya yataendelea kukaa Somalia hadi usalama utakapoimarishwa katika nchi hiyo iliyokumbwa na vita vya miaka mingi.

Jumanne, 1 Oktoba 2013

Jumanne, 01 Oktoba 2013 20:03 Iran: Obama akabiliane na wapenda vita

Iran: Obama akabiliane na wapenda vita



Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa viongozi wa Marekani wanapaswa kuamiliana na Iran kwa kutilia maanani uhakika wa mambo na kuliheshimu taifa la nchi hii

UN: Idadi ya wakimbizi wa Congo imeongezeka




Ripoti mpya iliyotolewa na Umoja wa Mataifa imesema kuwa idadi ya watu wanaokimbia vita na machafuko katika Jamhuri ya Kidemokrasia ay Congo imeongezeka na kuwa zaidi ya laki tatu na nusu katika miezi ya hivi karibuni.

Polisi 12 wa Msumbiji wahukumiwa kifungo jela


Polisi 12 wa Msumbiji wahukumiwa kifungo jela



Polisi 12 wa Msumbiji wahukumiwa kifungo jela

Mapigano makali yaendelea mashariki mwa Kongo




Mapigano makali yaendelea mashariki mwa Kongo

Kwa akali watu 10 wameuawa na makumi  ya wengine kujeruhiwa baada ya kujiri mapigano makali kati ya wapiganaji wa kundi la Alliance of Patriots for a Free and Sovereign Congo  APCLS na wanamgambo wa kundi la Sheka katika eneo la Kalembe mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.