Rais wa Marekani Barrack Obama amefuta ziara yake barani Asia na pia hatohudhuria mikutano miwili ya kimataifa kutokana na kufungwa kwa shughuli za serikali ya Marekani.
TANGAZO
WEKA TANGAZO LAKO HAPA
Jumamosi, 5 Oktoba 2013
Watu wanne wauwawa Mombasa
Watu wanne wamethibitishwa kuuwawa baada ya makabiliano makali kati ya polisi na waandamanaji mjini Mombasa kenya walioandamana hapo jana baada ya Sala ya Ijumaa kupinga kuuwawa kwa Sheikh Ibrahim Ismail
Shughuli za uokoaji zasimamishwa Lampedusa
Zaidi ya watu miamoja kumi na watu wamepatikana wakiwa wamekufa maji na wengine miambili bado hawajulikani waliko
Hali mbaya ya hewa imewasababisha waokoaji kuahirisha juhudi za kutafuta miili ya wahamiaji zaidi ya 200 ambao hawajulikani waliko, baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kushika moto na kuzama karibu na kisiwa cha Lampedusa, kusini mwa Italia. Wapiga mbizi walifanikiwa kuipata miili zaidi ya 100 ya wahamiaji huku watu zaidi ya 150 wameokolewa. Inaaminika boti hiyo iliopinduka ilikuwa na wahamiaji takriban 500 waliokuwa wanatokea nchini Somalia na Eritrea. Kamishna wa Umoja wa Ulaya anayeshughulika na maswala ya ndani Cecilia Malmstroem, ameapa kuwa atapambana na watu wanaosafirisha watu kwa njia haramu kwa kutumia hali yao mbali ya maisha. Italia ilitangaza siku moja ya maombolezo jana Ijumaa.
Wafuasi wa Morsi wakabiliana na polisi Misri
Idadi kubwa ya wafuasi wa Morsi wamezuiliwa na wengine kuuawa
Vikosi vya usalama nchini Misri vimeimarisha ulinzi katika sehemu kadhaa mjini Cairo baada ya vurugu kuzuka kutokana na makabiliano kati ya wafuasi wa Mohammed Morsi na vikosi vya usalama katika mji huo na ule wa Alexandria.
Mambo Shuari Rwanda na TZ, asema Kikwete
Rais wa TZ , Jakaya Kikwete
Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete ametangaza kuwa mgogoro baina ya Tanzania na Rwanda umemalizika.
Katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi kwa raia wa nchi hiyo Rais Kikwete amesema hatua hiyo inafuatia mazunguzo baina ya viongozi hao wawili yaliyofanyika hivi karibuni nchini Uganda
Ijumaa, 4 Oktoba 2013
Rwanda yakosoa vikwazo vya Marekani dhidi yake
Jeshi la Rwanda limekosoa vikali vikwazo vilivyowekwa na Marekani dhidi ya nchi hiyo. Taarifa zinasema kuwa, Marekani imechukua uamuzi huo baada ya kulituhumu jeshi la Rwanda kuwa liliwasaidia waasi wa M23 wa Kongo katika kuwatumikisha watoto jeshini.
Juhudi za uokozo zaendelea Lampedusa
Baadhi ya waliopoteza maisha yao wakitafuta kuingia Ulaya
Juhudu za uokozi zimeanza tena Kusini mwa Utaliano baada ya boti iliyokuwa imewabeba wahamiaji wa kiafrika kwenda Italia, kuzama katika kisiwa cha Lampedusa.
Jisajili kwenye:
Maoni
(
Atom
)