TANGAZO
WEKA TANGAZO LAKO HAPA
Jumanne, 1 Oktoba 2013
Mapigano makali yaendelea mashariki mwa Kongo
Kwa akali watu 10 wameuawa na makumi ya wengine kujeruhiwa baada ya kujiri mapigano makali kati ya wapiganaji wa kundi la Alliance of Patriots for a Free and Sovereign Congo APCLS na wanamgambo wa kundi la Sheka katika eneo la Kalembe mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Jumatatu, 30 Septemba 2013
Chuo kilichovamiwa Nigeria kilikosa ulinzi
Maafisa wa utawala nchini Nigeria wanasema kuwa hapakuwa na ulinzi katika chuo cha mafunzo ya kilimo nchini Nigeria ambako hadi wanafunzi 50 waliuawa Jumapili.
Wabunge, Kenya - wakimbizi waondolewe
Kamati ya bunge inayohusika na ulinzi na uhusiano na mataifa ya kigeni imependekeza kufungwa kwa kambi za wakimbizi nchini Kenya, ikisema zinatishia usalama wa nchi.
Jumapili, 29 Septemba 2013
Boko Haram yaua watu 27 Nigeria
Kundi la Boko Haram limeua watu wasiopungua 27 katika mashambulizi mawili tofauti yaliyofanyika huko kaskazini mwa Nigeria.
‘Hatari ya silaha za nyuklia za Israel izingatiwe’
Msemaji wa Jumuiya ya Kiislamu ya Colombia amesema kuwa, walimwengu wanapaswa kuzingatia hatari ya silaha za atomiki za utawala wa Kizayuni wa Israel. Rashid Caravali amesisitiza kwamba, umewadia wakati sasa kwa nchi za Mashariki ya Kati na nchi nyingine ulimwenguni kuipa uzito hatari ya silaha za nyuklia za utawala haramu wa Israel hasa kwa kuzingatia kwamba, utawala huo mara kadhaa wa kadhaa umeonesha wazi na bila kificho uadui wake kwa nchi za eneo. Msemaji wa Jumuiya ya Kiislamu ya Colombia ameongeza kuwa, Israel sio tu kwamba, inamiliki silaha za kemikali bali inazo pia silaha za nyuklia ambazo ni tishio kubwa kwa usalama wa dunia hususan eneo la Mashariki ya Kati. Rashid Caravali amesema, jamii ya kimataifa inapaswa kuushinikiza utawala huo ghasibu ili uangamize silaha zake zote za atomiki na kwa muktadha huo eneo la Mashariki ya Kati litashuhudia amani na utulivu.
Jisajili kwenye:
Maoni
(
Atom
)