TANGAZO

TANGAZO
WEKA TANGAZO LAKO HAPA

Ijumaa, 11 Oktoba 2013

Rais Banda awafuta kazi mawaziri kwa ufisadi

Rais Banda amewafuta kazi mawaziri wake wote kutokana na ufisadi
Rais wa Malawi, Joyce Banda amelifuta kazi baraza lake la mawaziri kutokana na kuongezeka kwa visa vya ufisadi serikalini.
Maafisa wa serikali wamekuwa wakipatikana na pesa zikiwa zimefichwa chini ya vitanda vyao na kwenye magari yao, kwa mujibu wa mwandishi wa BBC Raphael Tenthani.

Alhamisi, 10 Oktoba 2013

Taliban tayari kwa mazungumzo Pakistan

Taliban wako tayari kwa mazungumzo ila wataendelea kushambulia maslahi ya Marekani

Kiongozi wa Taliban nchini Pakistan Hakimullah Mehsud ameambia BBC kuwa yuko tayari kwa mazungumzo na serikali ingawa amesisitiza kuwa bado serikali haijamshauri.

Marekani kubana msaada wa kijeshi Misri

Marekani intaka Misri kuhakikisha uchaguzi huru na haki unafanyika kabla ya kuipa msaada tena
Marekani inabana sehemu kubwa ya dola bilioni 1.3 ambazo hutolewa kwa Misri kama msaada wa kijeshi.

Jumanne, 8 Oktoba 2013

peruuuuzi na kdadisi magazeti ya bongo ya leo j,4 octoba 13

 
 

Wanajeshi watano wauawa Misri

Kuna wasiwasi kuwa wanajeshi na vikosi vya usalama vinalengwa kwa mashambulizi la Misri
Watu waliojihami nchini Misri wamewaua wanajeshi watano katika eneo la Mkondo wa Suez mjini Ismailiya.

Lampedusa: Miili 232 imepatikana

Wanajeshi wakisaidia na juhudi za kuokoa maiti
Wapiga mbizi nchini Utaliana wamapeta idadi kubwa ya maiti katika boti iliyozama na ambayo ilikua imewabeba wahamiaji wa kiafrika kwenda Ulaya siku ya Alhamisi.

Jumapili, 6 Oktoba 2013

Maiti zaidi zapatikana Lampedusa

Kazi za uokozi zaanza tena Lampedusa

Wakuu wa Utaliana katika kisiwa cha Lampedusa wanasema wameopoa miili zaidi kutoka meli iliyozama Alkhamisi.