TANGAZO

TANGAZO
WEKA TANGAZO LAKO HAPA

Jumapili, 29 Septemba 2013

Kenya: Maafisa walikuwa na taarifa

Vikosi vya usalama vilipambana na magaidi wa Al Shabaab waliowaua wakenya wengi wasio na hatia

Mawaziri wa serikali walipokea taarifa kuhusu tisho la mashambulizi ya kigaidi kabla ya kundi la Al Shabaab kushambulia jengo la Westgate mjini Nairobi.
Kwa mujibu wa taarifa za kijasusi zilizofichuliwa, zilionyesha maelezo ya mipango ya mashambulizi hayo kufanyika Nairobi au mjini Mombasa.
Mawaziri wanne na mkuu wa majeshi walikuwa wamefahamishwa kuhusu tisho la kufanyika shambulizi la kigaidi.
Watu 67 walifariki na mamia kujeruhiwa katika shambulizi la kigaidi ambalo Al Shabaab walikiri kulifanya Septemba 21 mjini Nairobi.
Kwa mujibu wa taarifa za gazeti la Daily Nation, mawaziri walipokezwa taarifa za kati ta yarehe 13 na 20 kuhusu uwezekano wa kufanyika mashambulizi kadhaa ya kigaidi mjini Mombasa na Nairobi.
Onyo hizo zilitolewa kwa mara ya kwanza mnamo mwezi Januari kwa mujibu wa gazeti hilo na kwa mara nyingine kuanzia Septemba.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, serikali ya Israel pia ilitoa taarifa za kuonya kuwa huenda magaidi wakashambulia majengo yanayomilikiwa na raia wake kati ya tarehe 4 na 28 Septemba.
Daily Nation limeripoti kuwa taarifa za kijasusi zilionyesha kuwa viongozi wa al-Shabab walikuwa wameanza kulenga maeneo ya kushambulia ikiwemo Westgate na kanisa la Holy Family Basilica.
Kuna hofu idadi ya waliofariki huenda ikaongezeka.
Maafisa wa serikali wanaosemekana kupokea taarifa hizo ni pamoja na waziri wa fedha, Julius Rotich, waziri wa usalama Joseph Ole Lenku, waziri wa maswala ya kigeni, Amina Mohammed, waziri wa ulinzi Raychelle Omamo na mkuu wa majeshi Julius Karangi.
Mkuu wa shirika la ujasusi Michael Gichangi, anatarajiwa kuhojiwa na kamati ya bunge kuhusu usalama siku ya Jumatatu.

Jumamosi, 28 Septemba 2013

Kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya miaka 30, viongozi wa Marekani na Iran wamezungumza moja kwa moja.



Rais Rouhani na ObamaRais Rouhani na Obama

Rais Barack Obama na mwenzake wa Iran, Hassan Rouhani, wamezungumza kwa simu kwa muda wa robo saa; na kwa mujibu wa Bwana Obama walieleza azma yao ya kutatua mzozo wa muda mrefu kuhusu mradi wa nuklia wa Iran.
Ujumbe kwenye mtandao wa Twitter kutoka ofisi ya Bwana Rouhani ulionesha hisia kama hizo.
Taarifa kutoka Iran zinaonesha kuwa tukio hilo limefurahiwa nchini humo, hasa kati ya washauri wakuu wa Bwana Rouhani.

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda anatarajiwa kufungua Kongamano la siku mbili la Uwekezaji kanda ya Kaskazini kesho



wwwbinhafidhi.blogspot.com

WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda anatarajiwa kufungua Kongamano la siku mbili la   Uwekezaji kanda ya Kaskazini kesho pamoja na maonyesho ya kibiashara na Utalii ambapo wageni wa ndani na nje ya nchi wanatarajiwa kuhudhuria.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa alisema Pinda anatarajiwa kuwasili kesho (leo) ambapo jumla ya wageni 450 wanatarajiwa kuhudhuria.

Alisema Kongamano hilo la siku mbili litashirikisha halmashauri 33 za kanda ya Kaskazini ambapo kila moja itajifunza na kueleza namna ambavyo halmashauri yake inavyoendeshwa.

“Waziri Mkuu Mizengo Pinda ndie atakaeongoza kongamano letu la siku mbili pamoja na kufungua maonyesho ya kibiashara—hii  ni fursa nzuri ya  wenye viwanda na biashara kujitangaza” alisema na kuongeza

“Kongamano hili litakuwa na mapinduzi kwa halmashauri zetu hasa kwa hii kanda ya kaskazini kwani baada ya hapo tunataka kufanya kazi kwa vitendo na sio kwa nadharia” alisema Gallawa

Gallawa alisema kongamano hilo ambalo lengo lake ni kuwashawishi wawekezaji kujionea fursa zilizopo za uwekezaji kanda ya kaskazini  pamoja na miundombinu mizuri ya kusafirisha bidhaa kwa kutumia barabara, reli na bandari zikiwa zinapatikana.

Alisema Mikoa ya kanda ya Kaskazini iko na fursa nyingi za uwekezaji lakini inashindwa kujitangaza na hivyo kuonelea kuitisha kongamano hilo pamoja na wawekezaji kujionea wao wenyewe.

“Mimi nadhani baada ya kongamano hili wawekezaji watajua kuwa kweli eneo letu linafaa kwa uwekezaji na ninaamini maisha ya wananchi yatabadilika na umasikini utapungua” alisema Gallawa

Alisema kongamano hilo ambalo litaenda sambamba na maonyesho ya biashara na kazi za asili zinazotengenezwa  ndani na kuwataka wananchi kujifunza kupitia kongamano hilo ambalo ni nafasi adhimu kwao na kwa Mk

maalim seif afunguka kuhusu muungano

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF) Seif Sharrif Hamad amesema mgogoro wa Muungano uliopo unatokana na kufichwa kwa makubaliano yaliyowekwa na waasisi wa Muungano  na hivyo kusema kuwa kero hizo hazitokwisha hadi kuwepo kwa Serikali tatu na Muungano wa mkataba.

Aliyasema hayo juzi wakati wa kongamano la Wanzanzibar waishio Bara na kusema kuwa Muungano uliotiwa saini na waasisi wa Muungano huo umefichwa na hivyo kutaka dawa yake ni kuwepo kwa Serikali tatu na  Muungano wa mkataba.

Seif Sharif Hamad ambaye pia ni Makamo wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, alimtaka Rais Jakaya Kikwete kutosaini Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Mabadiliko ya Katiba 2013 kwa maelezo kuwa una kasoro.

“Wanzanzibar wenzangu mimi pia ni mmoja wa Wanzanzibar ambao tunataka Muungano wa mkataba---nilipoulizwa na tume nilisema nataka Muungano wa mkataba—nadhani nanyi pia mawazo yenu ni kama mimi” alisema Hamad

Hamad aliisifu Serikali ya Kikwete kwa kuwaachia wananchi  wenyewe kuiandika Katiba yao  na hivyo kumtahadharisha kutokuwa na wazo la kutia saini Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Mabadiliko ya Katiba 2013.

Alisema Zanzibar ni nchi kamili yenye mamlaka kama ilivyo kwa nchi nyengine hivyo inahitaji kurejeshewa mamlaka yake na kuwa na maamuzi ikiwa na pamoja kurejeshewa kiti chake katika Baraza la Umoja wa Kimataifa.

“Zanzibar iko na haki ya kuingia mikataba na jumuiya za kimataifa kama ilivyo nchi nyengine---tunataka dola ya Zanzibar iliyo nchi kamili kama ilivyokuwa zamani---Muungano umeifuta Zanzibar katika ramani ya kimataifa” alisema na kuongeza

“Hivi sasa Zanzibar haina haki ya kusema inajiunga na jumuiya yoyote ya kimataifa---kikwazo hiki ni kufichika kwa makubaliano ya Muungano kutoka kwa waasisi wetu ambao tunasema umefichwa” alisema Seif Sharif Hamad

Alisema ili kuondoa migogoro na manung’uniko za pande zote mbili ni kuwepo kwa Serikali tatu na Muungano wa mkataba jambo ambalo litaondosha kelele zote za Muungano na kupelekea ustawi wa jamii na  umoja na mshikamano miongoni mwa wananchi.

Kiongozi huyo aliwataka Wanzanzibar wanaoishi Bara kwa pamoja kushikamana na kutunza umoja wao na kuhakikisha Katiba Mpya inaweka madai yao likiwemo la kutaka Muungano wa mkataba.

sudan nako kwanuka hakukaliki

50 wauawa kwenye ghasia Sudan

wwwbinhafidhi.blogspot.com

Ghasia zilianza Jumatatu serikali ilipoondoa ruzuku kwa mafuta
Maafisa wa usalama nchini Sudan wamewaua watu 50 katika maandamano yaliyofanywa kwa siku kadhaa kupinga hatua ya serikali kuondoa ruzuku ya mafuta. Taarifa hii ni kwa mujibu wa mashirika ya kutetea haki za binadamu nchini humo.
Polisi waliwatupia gesi ya kutoa machozi waandamanaji zaidi siku ya Ijumaa.

Waandamanaji wameikosoa serikali ya Rais Omar al-Bashir kwa hatua hii na kumtaka aondoke mamlakani.Maafisa wanasema kuwa chini ya watu 29 wamefariki na kusema kuwa serikali ilikuwa haiwezi tena kumudu gharama ya ruzuku ya mafuta.
Taasisi ya elimu ya maswala ya haki na amani pamoja na shirika la Amnesty International zimesema kuwa watu wamepata majeraha ya risasi kwenye vifua na vichwa kulingana na jamaa, madaktari na waandishi wa habari.
Kijana mwenye umri wa miaka 14 alikuwa miongoni mwa waathiriwa wengi waliokuwa kati ya umri wa miaka 19-26. Waliongeza kusema kuwa mamia ya watu wamezuiliwa.
"Kuwaua kwa kuwapiga risasi watu kwenye vifua na vichwani ni ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu na Sudan lazima isitishe ghasia hizi mara moja,’’ alisema Lucy Freeman, Naibu mkurugenzi wa shirika la Amnesty International.
Duru za hospitalini zimeambia BBC kuwa takriban watu 60 wameuawa.
Maafis wa serikali ya Sudan bado hawajasema chochote kuhusu mauaji hayo lakini waziri wa habari Ahmed Belal Osman alisema kuwa idadi ya vifo ambayo ni juu zaidi ya watu 29 sio sawa.
Ghasia zilianza Jumatatu pale serikali ilipoondoa ruzuku kwa mafuta ili kupandisha ushuru. Hatua ya serikali kupunguza gharama ya matumizi ya pesa za umma, ilisababisha kupanda kwa bei ya mafuta na kuwaathiri sana watu wa kipato cha chini.

allwa mkubwa hatuna budi ya kumshukuru

dd
dunia ina mamboooooooooooooooooo hebu vuta pichaaaaaaaa kama ndo................................












Wakuu wa usalama kuhojiwa Kenya

hili ndio jengo la westgate nchini kenya  hapa ni ya sehem moja ya jengo hilo lilovyoporomoka


Maafisa wakuu wa ujasusi wametakiwa kufika mbele ya kamati ya ulinzi ya bunge ili kuhojiwa kuhusu mashambulizi ya kigaidi dhidi ya jumba la Westgate mjini Nairobi.
Taarifa kwenye vyombo vya habari nchini humo zinaonyesha kuwa hali ya kulaumiana imeanza kuibuka huku mashirika ya usalama yakinyosheana kidole.

Wataalamu wa uchunguzi wa mauaji wangali wanafanya uchunguzi wao wakitafuta miili na dalili za kilichosababisha shambulizi hilo.Watu 67 waliuawa kwenye shambulizi hilo huku zaidi ya miamoja sabini na tano wakipata majeraha mabaya. Shirika la Red Cross nalo linasema kuwa watu 61 wangali hawajulikani waliko.
Kamati ya bunge inataka maafisa wanaohusika na maswala ya usalama waweze kuwajibishwa.
Kundi la kigaidi la nchini Somalia, al-Shabab limedai kufanya mashambulizi hayo yaliyodumu siku nne kama hatua ya kulipiza kisasi kwa Kenya kujihusisha nchini Somalia kijeshi.
Hii leo ni siku ya tatu ya maombolezi kwa wathiriwa wa shambulizi hilo wakiwemo raia na wanajeshi.
Rais Uhuru Kenyatta amehudhuria mazishi ya mpwa wake na mchumba wake mjini Nairobi ambapo aliwahutubia waumini.

Walipuuza onyo?

Hatua ya kuwataka maafisa hao wa usalama kufika mbele ya tume ya bunge siku ya Jumatatu, inakuja kutokana na wasiwasi miongoni mwa wakenya kuhusu kiwango cha maafisa hao kujiandaa kwa tukio lolote la kigaidi sawa na lililotokea Westgate.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari mmoja wa maafisa waliotakiwa kufika mbele ya kamati hiyo ni mkuu wa shirika la ujasusi Michael Gichangi, anayesema alitoa taarifa za ujasusi kuhusu shambulizi hilo kwa polisi.
Lakini, afisaa mmoja mkuu katika idara ya polisi alikana kuwa taarifa hiyo ilitolewa kwa polisi.