TANGAZO

TANGAZO
WEKA TANGAZO LAKO HAPA

Alhamisi, 26 Septemba 2013

MAHAKAMA YAKATAA RUFAA YA TAYLOR



ALSHABAB MPAKA KIELEWEKE KENYA


Magaidi Tena Kenya, walipua kituo cha polisi, waua watu watatu, magari 11 yachomwa
Taarifa zilizotufikia hivi punde zinaeleza kuwa watu wanaozaniwa kuwa ni magaidi wamevamia kituo cha Polisi katika Mji wa Mandera nchini Kenya na kuwaua polisi wawili, watatu wamejeruhiwa vibaya na baadaye kuchoma magari zaid ya 11.

Ungana nasi baadaye kwa habari zaidi

Askari wa kulinda amani wa UN wabaka nchini Mali



Askari wa kulinda amani wa UN wabaka nchini Mali
Ripoti zinasema kuwa askari wasiopungua wanne wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wameshiriki katika ubakaji nchiniMali.
Askari hao ni miongoni mwa wanajeshi 1,500 wa Chad wanaohudumu katika Opereshini ya Kurejesha Amani ya Umoja wa Mataifa nchini Mali (MINUSMA).Tukio hilo limeripotiwa kutokea Septemba 19 ambapo wanajeshi hao walimbaka mwanamke mmoja katika mji wa kaskazini mwa Mali wa Gao. Umoja wa Mataifa umeitaka Chad kuchunguza suala hilo na kuwaadhibu wahusika.
Askari 6,000 wa Kiafrika walipelekwa kuhudumu katika kikosi cha kulinda amani nchini Mali, baada ya Ufaransa kuishambulia nchi hiyo Januari 11 mwaka huu kwa kisingizio cha kupambana na waasi wa kaskazini mwa Mali.

KENYA YAANZA KUCHUNGUZA SHAMBULIO LA WESTGATE



Kenya yaanza kuchunguza shambulio la Westgate


Mashirika ya kijasusi ya Marekani, Uingereza na Israel yanaisaidia Kenya kuchukunguza shambulio lililofanywa katika jengo la maduka la Westgate jijini Nairobi na kupelekea watu wasiopungua 72 kuuawa na kuharibiwa sehemu ya jengo hilo.

Afisa mwandamizi wa Kitengo cha Kitaifa cha Operesheni za Majanga amesema kuwa, uchunguzi huo ni kwa ajili ya kupata taarifa ambazo zitasaidia kufahamu utambulisho wa magaidi na uraia wao kikiwemo kipimo cha DNA.

Hayo yanajiri huku kundi la al Shabab lililotangaza kuhusika na shambulio la Nairobi likisema kwamba, shambulio la Westgate ni tahadhari kwa nchi za Magharibi na Kenya na kwamba, wanapaswa kuondoa askari wao nchini Somalia la sivyo watakabiliwa na umwagaji damu zaidi. Kwa mujibu wa Shirika la Msalaba Mwekundu la Kenya, zaidi ya watu 67 wameuawa wakiwemo maafisa sita wa Jeshi la Ulinzi la Kenya huku wengine karibu 200 wakijeruhiwa.
 

JK AWATAKA WAFADHILI WAACHE MANENO WATOE MZIGO WALIO AHIDI

Chapa
Rais Jakaya Kikwete,akizungumza kwenye mkutano uliojadili jinsi ya kuongeza kasi ya utekelezaji wa Malengo ya Milenia, New York, Marekani juzi.

Rais Jakaya Kikwete, amewataka wabia wa maendeleo wa nchi maskini kutimiza ahadi zao kama njia ya uhakika kuhakikisha Malengo ya Milenia yanayolenga kuzitoa nchi maskini kwenye uduni na kuziharakishia maendeleo.


Aidha, amesema Tanzania itatekeleza kwa ukamilifu baadhi ya malengo, lakini itakuwa vigumu kuyatelekeza yote manane kama inavyotakiwa chini ya Makubaliano ya Utekelezaji wa Malengo ya Milenia ifikapo mwaka 2015.


Aliyasema hayo alipozungumza kwenye mkutano uliojadili jinsi ya kuongeza kasi ya utekelezaji wa Malengo ya Milenia, New York, Marekani juzi.


Mkutano huo uliandaliwa na Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) na Benki ya Dunia (WB) kwenye Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York.


Rais Kikwete alisema kukawia kwa wafadhili hao kutoa fedha za utekelezaji wa malengo, kumechangia kwa kiasi fulani utekelezaji huo kutokuwa na kasi iliyotarajiwa kutokea mwanzo.


Hata hivyo, Rais Kikwete alisema pamoja na kucheleweshwa kwa fedha za kutosha za utekelezaji, Tanzania itaweza kwa kiasi fulani kufanikisha utekelezaji wa baadhi ya malengo, lakini ni dhahiri kuwa malengo mengine hayataweza kufikiwa ifikapo mwaka 2015 ambao ndiyo mwaka wa mwisho wa utekelezaji wa Malengo hayo.


Aliyataja Malengo hayo kuwa ni kufuta umaskini uliokithiri na njaa, kuinua kiwango cha afya na kupunguza vifo vya akinamama na watoto na kuhakikisha Tanzania inakuwa na mazingira endelevu.


mchakato wa Katiba Mpya bado kizungu mkuti


Harakati za kuuhamasisha umma kupinga mchakato wa mabadiliko ya katiba kuhodhiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) zimepamba moto, baada ya Waziri wa Katiba na Sheria wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Abubakari Khamisi Bakari, kuwataka Wazanzibari kutouunga mkono kwa madai kwamba, hawakushirikishwa.


Amesema iwapo serikali italazimisha mchakato wa mabadiliko ya Katiba kuendelea bila kuwashirikisha Wazanzibari katika kuutolea maoni Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wa Mwaka 2013, hawatakubali kwenda kwenye Bunge Maalum la Katiba.
Alisema hayo alipokuwa akihutubia maelfu ya watu katika mkutano wa hadhara, ambao ni mwendelezo wa harakati hizo, uliofanyika katika Uwanja wa Demokrasia Kibandamaiti, mjini hapa jana.


Harakati hizo zilizinduliwa na vyama vya CUF, Chadema, NCCR Mageuzi, katika viwanja vya Jangwani, jijini Dar es Salaam, Jumamosi wiki iliyopita.
Alisema Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai; Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, wamewahadaa Wazanzibari na kuudanganya umma kwamba, Wazanzibari walishirikishwa katika kuutolea maoni muswada huo wakati si kweli.


Aliwataka wabunge kutumia kanuni za Bunge kumchukulia hatua Ndugai kwa kulidanganya Bunge, vinginevyo awajibike kwa kujiuzulu.
Alisema pia kitendo cha Waziri Chikawe kueleza kwamba, Wazanzibari walishirikishwa katika kuutolea maoni Muswada huo, kimeonyesha kuwa ni mwongo. 


Bakari alisema Wazanzibari hawakushirikishwa katika hilo, badala yake kilichofanywa na serikali pamoja na Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria ni kuilaghai Zanzibar.
Alisema awali, Wazanzibari walipelekewa marekebisho ya muswada huo yakiwa na vifungu vinne pekee wakitakiwa wavitolee maoni.


Kwa mujibu wa Waziri Bakari, yeye binafsi alivipitia vifungu hivyo na kushauriana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) kabla ya kuvitolea maoni.
Alisema baada ya kuvipitia vifungu hivyo, alimwandikia barua Makamu wa Pili wa Rais wa SMZ, Balozi Seif Ali Iddi, na kumueleza kwamba, hawana matatizo na vifungu hivyo.


Alisema baada ya kumueleza hivyo Makamu huyo wa Rais, naye (Makamu wa Rais) alimwandikia Waziri Mkuu barua kumueleza maoni hayo ya Wazanzibari kuhusu vifungu hivyo.
Alisema hata hivyo, kitendo hicho cha Makamu wa Pili wa Rais wa SMZ, kilikuwa ni hadaa, kwani baadaye, walikwenda wakarekebisha vifungu 12 na kuvipeleka bungeni bila kuwashirikisha Wazanzibari kuvitolea maoni.


Alisema kitendo cha Ndugai kuwaonyesha wabunge bungeni barua hiyo ya Makamu wa Pili wa Rais wa SMZ na kusema kuwa Wazanzibari walishirikishwa kimeonyesha kuwa ni mwongo.
Alisema Wazanzibari walishirikishwa katika kuvitolea maoni vifungu vinne tu vya Muswada huo, lakini hawakushirikishwa kabisa katika kuvitolea maoni vifungu 12.


Alisema baadaye Chikawe na Lukuvi, walikweda Zanzibar kumuona (Waziri Bakari) wakitaka wajadili vitu vingine bila kuwapa muswada, hivyo akalikataa hilo kwa maelezo kwamba, hayuko tayari kuiuza Zanzibar. 


“Halafu wanatoka hapa wanakwenda kudanganya bungeni kwamba, waliwashirikisha Wazanzibari, waongo hawakutushirikisha,” alisema Waziri Bakari.
Alisema wanaupinga Muswada huo kwa kuwa kuna vifungu vinawaumiza Wazanzibari, ikiwamo kiwango cha wapigakura Wazanzibari kuipitisha Rasimu ya Katiba.


“Hivyo, itapita katiba ile  ile wanayoitaka CCM. hayo hatuyakubali hata kidogo. Hatukushirikishwa, katiba hii itawaumiza. Na yeyote Mzanzibari atakayeikubali hana akili,” alisema.
Aliwataka Wazanzibari kutoikubali rasimu hiyo na kusema kama serikali italazimisha basi hawatakubali kwenda kwenye Bunge la Katiba.


Mbunge wa Mkoani (CUF), Ali Khamis, alisema serikali haiko wazi katika kuendesha mchakato huo, hivyo akawataka wananchi kuwaunga mkono kuupinga.  Mkurugenzi wa Katiba na Sheria wa Chadema, ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, alisema bila katiba mpya hakuna Zanzibar huru na pia bila Zanzibar mpya hakuna katiba huru.


Alisema tangu mwaka 1964, Zanzibar imenyangánywa sauti yake katika Muungano.
 Lissu alisema wananchi wa Tanganyika na Zanzibar  hawakuulizwa kwa njia yoyote nchi hizo kuungana.
Lakini alisema baada ya miaka hiyo, leo Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linataka kutunga  katiba bila kuwashirikisha Wazanzibari.


Alisema pia kwa miaka yote mambo ya Muungano yameongezwa bila kuwashirikisha Wazanzibari, lakini wakipewa vyeo, au kuwekwa vizuizini wananyamaza.
 Lissu alisema ilipofika miaka ya 1984, walipoona Wazanzibari wanakuja juu, walianza kutumia mabavu kuwanyamazisha.


“Hivyo, kilichotokea Dodoma siyo kitu kigeni, ni mwendelezo wa mambo ya miaka 1960," alisema Lissu na kuongeza kuwa mambo hayo hayatakoma bila kuiondoa CCM madarakani.
Lissu alisema Dodoma wamechakachua sana na kusema iwapo Wazanzibari watanyamaza basi watakumbana na masaibu mbalimbali, ikiwamo kupunjwa idadi ya wajumbe watakaounda Bunge Maalum la Katiba na hivyo, kushindwa kujinusuru na unyongaji unaofanywa na serikali ya CCM dhidi yao.


Alisema pia iwapo wataruhusu na kufika hadi kwenye hatua upigaji kura ya maoni, basi watachakachuliwa kupitia Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC).
Mbunge wa Mkanyageni (CUF), Mohammed Habib Mnyaa, alisema kinachotaka kufanywa na CCM ni kutaka kuvuruga mchakato wa serikali tatu.
ALICHOSEMA MBATIA


Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, alisema tunu za Watanzania ni pamoja na utu, uzalendo, uwazi na lugha ya taifa, hivyo aliwataka kuhakikisha inapatikana katiba itakayoridhiwa na wote.
Alimuomba Rais Jakaya Kikwete kuzingatia ushauri uliotolewa na Waziri Bakari kwa kutosaini Muswada huo na kurudishwa bungeni ili ufanyiwe marekebisho ili kuliunganisha taifa.

MBOWE ANENA

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, alisema wamegundua Muungao ni mradi, ambao unatumiwa na kikundi cha watu wachache walioko Tanzania Bara na wengine Zanzibar.
Hivyo, akawataka Wazanzibari kuungana na wenzao wa Dar es Salaam, ambao alisema wamekubali kushiriki ama katika maandamano au mgomo unaoweza kuitishwa nchini kote Oktoba 10, mwaka huu, kudai katiba inayotakiwa na wananchi wote.


KAULI YA LIPUMBAMwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, alisema anamsikitikia Balozi Iddi kwa kukubali kushiriki katika kulidanganya Bunge kwamba, Wazanzibari walishirikishwa katika kuutolea maoni muswada huo, akisema kitendo hicho ni sawa na yeye alichakachuliwa bungeni.
Alisema kinachofanywa na wasaidizi wa Rais Kikwete ni  kumtakia mabaya, kwa kuwa iwapo atausaini muswada huo na kuwa sharia, mchakato wa katiba utakuwa umekwisha.
“Hivyo, tusikubali watu wachache wakatuzuia kupata katiba  inayoridhiwa na inayotokana na wananchi wenyewe,” alisema Profesa Lipumba.


HOJA ZA WAPINZANIKwa mujibu wa Lissu, wanachopinga katika muswada huo ni mapendekezo ya kumpa Rais mamlaka ya kuteua wajumbe 166 wa Bunge Maalum la Katiba kwani mapendekezo haya yanarudisha dhana kwamba wajumbe hao watakuwa watu wa Rais ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM.

“Rais Kikwete na chama anachokiongoza ni wadau wakubwa wa mchakato wa Katiba Mpya na wana maslahi halisi na makubwa ya kuhakikisha kwamba matakwa ya chama chao ndio yanakuwa Katiba Mpya ya nchi yetu, sasa anapopewa mamlaka ya kuteua wajumbe wa Bunge la Katiba inakuwa siyo sahihi ni wazi kuwa katiba mpya itakuwa ya Ki-CCM…CCM,” anasema.


Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, anasema hoja ya pili ambayo wanaipinga ni shinikizo kutoka kwa wabunge wa CCM ambao wanataka Tume ya Mabadiliko ya Katiba kuvunjwa, jambo ambalo wanaliona halina nia njema kwani wanaamini linatokana na chama tawala kutofurahishwa na Rasimu ya kwanza ya katiba iliyoandaliwa na tume hiyo.


Alisema wanashtushwa na uamuzi huo kwa sababu wabunge walipitisha bajeti ya Sh. bilioni 34 kwa ajili ya kuiwezesha tume hiyo kukamilisha mchakato wote wa katiba sasa wabunge wa CCM wanapopitisha sheria ya kuitaka tume ivunjwe siyo jambo zuri.
Hoja ya tatu ni kuhusu uwakilishi katika Bunge Maalum la Katiba, ambayo kwa mujibu wa Lissu, hakuna uwiano kati ya Tanzania Bara na Visiwani wakati Zanzibar nayo ni nchi, hivyo wananchi walitegemea kuwa na idadi sawa ya wajumbe katika bunge hilo.


“Wabunge wanaotoka Zanzibar katika Bunge la Jamhuri ya Muungano ni 83 wakati Baraza la Wawakilishi Zanzibar lina wajumbe 76. Kwa hiyo, ili kutekeleza matakwa ya kifungu cha 22(1) na (2) cha Sheria, Zanzibar itakuwa na wajumbe 219 katika Bunge Maalum lenye wajumbe 604, sawa na takriban asilimia 36 ya wajumbe wote wakati Tanzania bara watakuwa ni asilimia 64,” anasema.Anasema kwa kuwa inatengenezwa katiba ya nchi mbili, kunahitajika kuwa na uwiano sawa wa wajumbe kwenye Bunge la Katiba.

 

Rais Kikwete ana kwa ana na Melinda Gates